Jeshi la Uganda lakanusha taarifa za kuingia Kenya.

In Kimataifa

Jeshi la Uganda limekanusha taarifa kuwa liko tayari kuingia nchini Kenya, kusaidia kudhibiti hali ya usalama baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu nchini humo.

Katika uchaguzi huo rais Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi, huku mpinzani wake mkuu Raila Odinga akiyapinga matokeo hayo.

Waziri wa mawasiliano nchini Uganda Frank Tumwebaze, amesema jeshi la Uganda haliwezi kutumwa nje ya nchi hiyo, kushiriki operesheni ya kijeshi kisiri.

Msemaji wa jeshi la Uganda Richard Karemire amesema kuwa, Kenya ni nchi huru na usalama wake umo chini ya serikali ya nchi hiyo.

Aidha amesema Uganda haijapokea ombi lolote kutoka kwa Kenya, kutuma majeshi yake nchini humo au kuomba usaidizi.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu