Jeshi la Uganda lakanusha taarifa za kuingia Kenya.

In Kimataifa

Jeshi la Uganda limekanusha taarifa kuwa liko tayari kuingia nchini Kenya, kusaidia kudhibiti hali ya usalama baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu nchini humo.

Katika uchaguzi huo rais Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi, huku mpinzani wake mkuu Raila Odinga akiyapinga matokeo hayo.

Waziri wa mawasiliano nchini Uganda Frank Tumwebaze, amesema jeshi la Uganda haliwezi kutumwa nje ya nchi hiyo, kushiriki operesheni ya kijeshi kisiri.

Msemaji wa jeshi la Uganda Richard Karemire amesema kuwa, Kenya ni nchi huru na usalama wake umo chini ya serikali ya nchi hiyo.

Aidha amesema Uganda haijapokea ombi lolote kutoka kwa Kenya, kutuma majeshi yake nchini humo au kuomba usaidizi.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu