Joaon Lourenco atangazwa kuwa Rais mpya Angola.

In Kimataifa

Tume ya uchaguzi nchini Angola imesema chama tawala cha MPLA kimeshinda uchaguzi wa wiki hii na Joao Lourenco atakuwa rais mpya wa nchi hiyo.

Huku matokeo kamili yakitarajiwa kutolewa baadaye leo, maafisa wa tume wamesema chama cha MPLA kina uongozi mkubwa dhidi ya wapinzani wake baada ya tuluthi mbili ya vituo vote vya kupigia kura kuripoti matokeo yao.

Viongozi wa upinzani wanalalamika kwa kunyimwa fursa ya kuzungumza na vyombo vya habari ili kupambana katika uchaguzi huo kwa njia sawa, wakati kukiwa na mgogoro wa kiuchumi ambao umesababisha mfumko wa bei kupanda kwa asilimia 40.

Lourenco sasa atachukua nafasi ya Jose Eduardo Dos Santos, kiongozi aliyekosolewa sana katika uongozi wake wa miaka 38.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu