Joaon Lourenco atangazwa kuwa Rais mpya Angola.

In Kimataifa

Tume ya uchaguzi nchini Angola imesema chama tawala cha MPLA kimeshinda uchaguzi wa wiki hii na Joao Lourenco atakuwa rais mpya wa nchi hiyo.

Huku matokeo kamili yakitarajiwa kutolewa baadaye leo, maafisa wa tume wamesema chama cha MPLA kina uongozi mkubwa dhidi ya wapinzani wake baada ya tuluthi mbili ya vituo vote vya kupigia kura kuripoti matokeo yao.

Viongozi wa upinzani wanalalamika kwa kunyimwa fursa ya kuzungumza na vyombo vya habari ili kupambana katika uchaguzi huo kwa njia sawa, wakati kukiwa na mgogoro wa kiuchumi ambao umesababisha mfumko wa bei kupanda kwa asilimia 40.

Lourenco sasa atachukua nafasi ya Jose Eduardo Dos Santos, kiongozi aliyekosolewa sana katika uongozi wake wa miaka 38.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu