Jopo la Madaktari bingwa kutoka Marekani waendelea kuwafanyia matibabu wanafunzi majeruhi watatu.

In Kitaifa

JOPO la Madaktari bingwa kutoka Marekani, Hospitali ya Taifa ya Rufaa Muhimbili – MOI ya Dar es Salaam na Mount Meru ya mkoani Arusha ,wameendelea kuwafanyia matibabu kwa kina wanafunzi majeruhi watatu wa ajali ya Basi la Shule ya Lucky Vincent.

Mbali na uchunguzi huo wanafunzi hao watatu ambao kwa sasa wameendelea kuimarika, shughuli nyingine zilizofanyika jana zilikuwa ni kwa upande wa wazazi wa watoto na watoto wenye kujaza fomu, kwa ajili ya taratibu za Hati ya kusafiria.

Serikali kwa kushirikiana na jopo hilo la madakari bingwa kutoka Marekani, wameendelea na taratibu za kuwasafirisha majeruhi hao ambao ni Geofrey Tarimo, Sadia Awadhi na Doreen Mshanga, kwa ajili ya matibabu zaidi nchini Marekani.

Akizungumza mjini hapa  Mbunge wa Singida Kaskazini (CCM), Lazaro Nyalandu, aliyekuwa mwenyeji wa Madaktari waliotembelea jimboni kwake kisha kuelekea Ngorongoro amesema, taratibu zinaendelea za kuhakikisha watoto hao wanatibiwa.

Aidha amesema hadi  jana  hatua iliyokuwa ikiendelea chini ya uratibu wake, ilikuwa ni Shirika hilo la Madaktari wa Stemm kutoka Marekani kupata hospitali itakayowapokea watoto hao.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu