Jopo la Madaktari bingwa kutoka Marekani waendelea kuwafanyia matibabu wanafunzi majeruhi watatu.

In Kitaifa

JOPO la Madaktari bingwa kutoka Marekani, Hospitali ya Taifa ya Rufaa Muhimbili – MOI ya Dar es Salaam na Mount Meru ya mkoani Arusha ,wameendelea kuwafanyia matibabu kwa kina wanafunzi majeruhi watatu wa ajali ya Basi la Shule ya Lucky Vincent.

Mbali na uchunguzi huo wanafunzi hao watatu ambao kwa sasa wameendelea kuimarika, shughuli nyingine zilizofanyika jana zilikuwa ni kwa upande wa wazazi wa watoto na watoto wenye kujaza fomu, kwa ajili ya taratibu za Hati ya kusafiria.

Serikali kwa kushirikiana na jopo hilo la madakari bingwa kutoka Marekani, wameendelea na taratibu za kuwasafirisha majeruhi hao ambao ni Geofrey Tarimo, Sadia Awadhi na Doreen Mshanga, kwa ajili ya matibabu zaidi nchini Marekani.

Akizungumza mjini hapa  Mbunge wa Singida Kaskazini (CCM), Lazaro Nyalandu, aliyekuwa mwenyeji wa Madaktari waliotembelea jimboni kwake kisha kuelekea Ngorongoro amesema, taratibu zinaendelea za kuhakikisha watoto hao wanatibiwa.

Aidha amesema hadi  jana  hatua iliyokuwa ikiendelea chini ya uratibu wake, ilikuwa ni Shirika hilo la Madaktari wa Stemm kutoka Marekani kupata hospitali itakayowapokea watoto hao.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu