JPM aagiza kujengwa uzio kulizunguka eneo la Mererani.

In Kitaifa, Uchumi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ameamuru eneo la Mererani Block A hadi D ujengwe ukuta wenye mlango mmoja na kamera zifungwe ili kuweza kukabiliana na wizi wa madini aina ya Tanzanite.

Ameyasema hayo hii leo Septemba 20, 2017 kwenye ziara ya kikazi mkoani Manyara katika Wilaya ya Simanjiro ambapo amesema ujenzi wa ukuta huo utasaidia kuondokna na wizi madini hayo hivyo serikali itaweza kukusanya mapato yake kikamilifu.

Rais Magufuli ametoa tamko la soko la Tanzanite kuwa litakua Simanjiro na si Arusha kama ilivyozoeleka na kusema wanunuzi watatakiwa kufunga safari kuelekea Simanjiro.

Na Rais Magufuli pia kabla ya kuzindua barabara mkoani Mannyara amewaomba wananchi hao kuitumia barabara hiyo ipasavyo bila kuiharibu kwani ni ya kila mmoja na kuwaomba wale wanaendesha vyombo vya moto kasi kutofanya hivo.

Rais Magufuli kwa upande mwingine ametoa hofu wakazi wa simanjiro kuhusiana na swala la maji wamuachie yeye kwani atahusika nalo.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu