JPM awaapisha viongozi wapya wateule.


Leo June 22 2020 taarifa kutoka Ikulu jijini Dar Es Salaam ni
kuhusiana na kuapishwa kwa viongozi wapya wa Mkoa wa
Morogoro na Arusha akiwemo Mkuu wa Mkoa mpya wa Arusha
Mh Idd Hassan Kimanta pamoja na Mkuu wa Wilaya wa
Arusha Mh Kenan Kihongosi na Mkurugenziwa Arusha lakini
pia kwa upande wa Monduli Mkuu wa wilaya mpya ni ACP
Edward Balele na Morogoro Mkuu wa Wilaya mpya ni Bakari
Msulwa ,Rais Magufuli ametaja sababu za kutengua viongozi
wa Mkoani Arusha huku pia

Kwa upande mwingine Rais Magufuli amewataka IGP na RC
kuwaonya watendaji wa Mkoa wa Arusha kwa lengo la kufanya
kazi walizotumwa na Mh Rais na kutofanya kazi ambazo Mh
Rais hajawatuma huku Mh Rais Magufuli akisema leo ilibidi
awatoe RPC na Mkuu wa TAKUKURU wa Arusha ila
ameonelea kuwaonya na kusema amewasamehe ila

hajawasamehe moja kwa moja kwani wakifanya kosa
wataondoka.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mh Suleiman
Jaffo baada ya kiapo kwa viongozi hao wapya wateule amesema
viongozi hao hawanabudi kumtanguliza Mungu katika
uchapakazi wao na kufanya yale waliyoagizwa kufanya na si
vinginevyo huku akisisitiza ushirikiano katika kila idara na si
mabishano.

Baada ya kula kiapo Mkuu wa Mkoa mpya wa Arusha Mh Idd
Hassan Kimanta amesema atafanyakazi kwa misingi na malengo
huku akimshukuru Rais Magufuli kwa kumpatia nafasi hiyo.

Exit mobile version