Kagame tayari anadai kuwa mshindi katika uchaguzi ujao wa rais utakaofanyika tarahe nne mwezi ujao.

In Kimataifa

Rais wa Rwanda Paul Kagame tayari anadai kuwa mshindi katika uchaguzi ujao wa rais utakaofanyika tarahe nne mwezi ujao.

Kagame jana aliwaambia wafuasi wake katika mkutano wa kwanza wa kuanza rasmi kwa kampeini nchini humo kuwa matokeo ya uchaguzi tayari yalijulikana mnamo mwaka 2015 wakati zaidi ya Wanyarwanda milioni nne waliposhiriki katika kura ya maoni ili bunge kuifanyia katiba mageuzi ya kumruhusu kugombea muhula mwingine madarakani.

Kagame amesema wapinzani wake hawawezi kubadilisha mapenzi ya wananchi kuwa yeye ndiye chaguo pekee kwa warandwa.

Rais huyo wa Rwanda amekuwa madarakani tangu kukamilika kwa mauaji ya halaiki yaliyoikumba nchi hiyo mwaka 1994,Licha ya kuwa anasifiwa kwa kuleta uthabiti katika taifa hilo la takriban watu milioni 12.

Aidha anashutumiwa na mashirika ya kutetea haki za binadamu kwa kutumia mkono wa chuma kuliongoza taifa na kuwakandamiza wapinzani nchini humo.

Wagombea wengine wa urais ni Frank Habineza wa chama cha Democratic Green na mgombea huru Philippe Mpayimana.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu