Kagame tayari anadai kuwa mshindi katika uchaguzi ujao wa rais utakaofanyika tarahe nne mwezi ujao.

In Kimataifa

Rais wa Rwanda Paul Kagame tayari anadai kuwa mshindi katika uchaguzi ujao wa rais utakaofanyika tarahe nne mwezi ujao.

Kagame jana aliwaambia wafuasi wake katika mkutano wa kwanza wa kuanza rasmi kwa kampeini nchini humo kuwa matokeo ya uchaguzi tayari yalijulikana mnamo mwaka 2015 wakati zaidi ya Wanyarwanda milioni nne waliposhiriki katika kura ya maoni ili bunge kuifanyia katiba mageuzi ya kumruhusu kugombea muhula mwingine madarakani.

Kagame amesema wapinzani wake hawawezi kubadilisha mapenzi ya wananchi kuwa yeye ndiye chaguo pekee kwa warandwa.

Rais huyo wa Rwanda amekuwa madarakani tangu kukamilika kwa mauaji ya halaiki yaliyoikumba nchi hiyo mwaka 1994,Licha ya kuwa anasifiwa kwa kuleta uthabiti katika taifa hilo la takriban watu milioni 12.

Aidha anashutumiwa na mashirika ya kutetea haki za binadamu kwa kutumia mkono wa chuma kuliongoza taifa na kuwakandamiza wapinzani nchini humo.

Wagombea wengine wa urais ni Frank Habineza wa chama cha Democratic Green na mgombea huru Philippe Mpayimana.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu