Kamati maalum yapokelewa kwa mabango-Mererani

In Kitaifa

Wachimbaji wadogo wa madini ya Tanzanite katika migodi ya Mererani wameipokea kwa mabango kamati maalum ya bunge iliyoundwa na spika wa Bunge Job Ndugai kuchunguza mwenendo mzima wa madini ya Tanzanite ambapo baadhi ya mabango yamebeba ujumbe wa kuiomba serikali kuangalia upya sheria ya uchimbaji katika eneo hilo ili kupunguza migogoro baina ya wachimbaji wadogo na wakubwa.

Wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe mbalimbali wachimbaji hao wamepaaza sauti zao mbele ya kamati maalumu ya bunge ya kuchunguza mwenendo mzima wa madini ya tanzanite ambayo iko katika eneo hilo ikitekeleza baadhi ya majukumu yake ambapo ilipata nafasi ya kuzungumza na makundi yote muhimu kwa nyakati tofautitofauti.

Mwenyekiti wa kamati hiyo Dotto Biteko analazimika kutoa ufafanuzi kidogo juu ya kazi na majukumu ya kamati hiyo huku akiwataka wachimbaji hao kuwa na subira mpaka pale kamati hiyo itakapokamilisha kazi yake ikiwemo kuandaa, kuchunguza na kutoa ushauri kwa serikali nini kifanyike dhidi ya kile ilicho kibaini baada ya uchunguzi wake.

Moja ya hadidu za rejea za kamati hiyo maalum ni kupitia mkataba uliopo baina ya shirika la taifa la madini STAMICO na Tanzanite One na kuangalia ushiriki wa Sky Associates ili kuona manufaa ambayo nchi inapata kutokana na biashara ya madini hayo.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu