KAMISHNA WA TUME HURU YA UCHAGUZI NA MIPAKA (IEBC) AJIUZULU.

In Kimataifa


Kamishna wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) nchini Kenya, Dk Roselyn Akombe ametangaza kujiuzulu nafasi yake katika tume hiyo.

Dk Akombe ametuma taarifa ya kujiuzulu akiwa mjini New York nchini Marekani anakoishi ambapo alikuwa akiufanyia kaziUmoja wa Mataifa kabla ya kujiunga na tume ya IEBC.

Katika taarifa yake, Akombe amesema kwamba uchaguzi wamarudio wa uraisi uliopangwa kufanyika Oktoba 26 mwaka huu haujafikia vigezo vya kuwa uchaguzi huru na wa haki.

Akombe anajiondoa kwenye tume hiyo ya IEBC ikiwa imebakiwiki moja uchaguzi wa urais kurudiwa kutokana na matokeo ya awali kufutwa na mahakama kuu na kuamuru uchaguzi mpyaufanyike.

Agosti Akombe alizuiliwa kwenye uwanja wa ndege wa JKIA akielekea nchini Marekani.

Dk Roselyn Akombe Kwamboka alizaliwa 1976 katika kaunti ya Nyamira , na kusomea katika chuo kikuu cha Nairobi kabla yakuelekea nchini Marekani kwa masomo zaidi.

Ana shahada ya uzamifu katika masuala ya sayansi na kimataifa mbali na shahada nyengine kama hiyo katika somo hilo kutoka chuo kikuu cha Rutgers .

Hadi uteuzi wake katika tume hiyo alifanya kazi kama katibu katika Umoja wa Mataifa mjini New York, wadhfa ambao anasema ulimwezesha kuwa na uzoefu katika maswala hayo na uwezo wake mkuu amesema mbele ya kamati ya bunge nchini Kenya, ni kutatua migogoro na kwamba ameishi ng’ambo kwa takriban miaka 15,hatua iliomwezesha kuelewa zaidi mahitaji ya watu wanaoishi ughaibuni wakati wa uchaguzi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu