Kansela wa Austria awahimza washirika wa muungano wa kihafidhina kubaki serikalini baada ya kiongozi muungano huo kujiuzulu.

In Kimataifa

  Kansela wa Austria Christian Kern amewahimiza washirika wa muungano wake wa kihafidhina kubakia serikalini baada ya kiongozi wa muungano huo kujiuzulu kwa ghafla, na kuongeza uwezekano wa kuitishwa uchaguzi wa mapema wakati chama cha siasa kali za mrengo wa kulia kikiongoza katika uchunguzi wa maoni.

Uchaguzi mpya unaweza kukipa chama kinachopiga sera za uhamiaji cha Freedom Party – FPO nafasi ya kuingia katika serikali ya kitaifa ikiwa ni chini ya mwaka mmoja baada ya mgombea wake kushindwa katika kinyang’anyiro kikali cha urais.

Naibu wa Kansela Reinhold Mittelana, kiongozi wa chama cha kihafidhina cha People’s Party – OVP alisema mapema jana kuwa anajiuzulu baada ya kushindwa kutuliza malumbano ndani ya chama na uvumi kuhusu uongozi wa usoni wa chama hicho.

Waziri wa Mambo ya Kigeni Sebastian Kurz ambaye ana umri wa miaka 30 huenda akachukua wadhifa huo.

Viongozi wa chama cha OVP watakutana Jumapili ijayo kumtafuta mrithi wa Mitterlehner

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu