Kansela wa Austria awahimza washirika wa muungano wa kihafidhina kubaki serikalini baada ya kiongozi muungano huo kujiuzulu.

In Kimataifa

  Kansela wa Austria Christian Kern amewahimiza washirika wa muungano wake wa kihafidhina kubakia serikalini baada ya kiongozi wa muungano huo kujiuzulu kwa ghafla, na kuongeza uwezekano wa kuitishwa uchaguzi wa mapema wakati chama cha siasa kali za mrengo wa kulia kikiongoza katika uchunguzi wa maoni.

Uchaguzi mpya unaweza kukipa chama kinachopiga sera za uhamiaji cha Freedom Party – FPO nafasi ya kuingia katika serikali ya kitaifa ikiwa ni chini ya mwaka mmoja baada ya mgombea wake kushindwa katika kinyang’anyiro kikali cha urais.

Naibu wa Kansela Reinhold Mittelana, kiongozi wa chama cha kihafidhina cha People’s Party – OVP alisema mapema jana kuwa anajiuzulu baada ya kushindwa kutuliza malumbano ndani ya chama na uvumi kuhusu uongozi wa usoni wa chama hicho.

Waziri wa Mambo ya Kigeni Sebastian Kurz ambaye ana umri wa miaka 30 huenda akachukua wadhifa huo.

Viongozi wa chama cha OVP watakutana Jumapili ijayo kumtafuta mrithi wa Mitterlehner

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu