Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) amemlaumu msajili wa vyama vya Siasa.

In Kitaifa
Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Sharif Hamad Seif amemlaumu msajili wa vyama vya Siasa nchini Jaji Francis Mutungi kwa kushirikiana na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) kwa kuunda bodi ya wadhamini feki wa chama hicho.
Ameyasema hayo jana Jijini Dar es salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, amesema kuwa wamefanya hivyo ili kuweza kumsaidia Prof. Lipumba ambaye alijiuzuru kwa matakwa yake mwenyewe.
Amesema kuwa RITA imepata shinikizo  kusajili wajumbe feki wa Bodi ya wadhamini wa CUF kwa kutumia majina yaliyowasilishwa na Prof. Ibrahimu Lipumba ili kuhujumu majina halali yaliyopitishwa na Baraza Kuu la Uongozi wa la Taifa kupitia kikao chake kilichofanyika makao makuu ya chama Zanzibar.
Hata hivyo, ameongeza kuwa hujuma iliyofanywa na RITA kwa kushirikiana na Msajili wa vyama vya Siasa nchini na Prof. Lipumba haiwezi kusaidia chochote katika kukiimarisha chama hicho

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu