Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) amemlaumu msajili wa vyama vya Siasa.

In Kitaifa
Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Sharif Hamad Seif amemlaumu msajili wa vyama vya Siasa nchini Jaji Francis Mutungi kwa kushirikiana na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) kwa kuunda bodi ya wadhamini feki wa chama hicho.
Ameyasema hayo jana Jijini Dar es salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, amesema kuwa wamefanya hivyo ili kuweza kumsaidia Prof. Lipumba ambaye alijiuzuru kwa matakwa yake mwenyewe.
Amesema kuwa RITA imepata shinikizo  kusajili wajumbe feki wa Bodi ya wadhamini wa CUF kwa kutumia majina yaliyowasilishwa na Prof. Ibrahimu Lipumba ili kuhujumu majina halali yaliyopitishwa na Baraza Kuu la Uongozi wa la Taifa kupitia kikao chake kilichofanyika makao makuu ya chama Zanzibar.
Hata hivyo, ameongeza kuwa hujuma iliyofanywa na RITA kwa kushirikiana na Msajili wa vyama vya Siasa nchini na Prof. Lipumba haiwezi kusaidia chochote katika kukiimarisha chama hicho

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu