Katibu Mkuu wa (CUF) afanya ziara kimya kimya Jijini Dar es salaam,kwa kutembelea wagonjwa na kutoa pole kwa wafiwa

In Kitaifa
   KATIBU Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, amefanya ziara kimya kimya jijini Dar es Salaam, kwa kutembelea wagonjwa na kutoa pole kwa wafiwa wa chama hicho.
Ziara hiyo ameifanya huku akiwa ameongozana na baadhi ya viongozi wa chama hicho akiwamo Mbunge wa Temeke, Abdalah Mtolea (CUF), Naibu Meya wa Jiji, Mussa Kafana na Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omar Kumbilamoto.
Katibu mkuu huyo alifanya ziara hiyo katika kata za Gongolamboto, Majohe, Kigamboni na Upanga, ambapo alizungumza na wananchi mbalimbali aliowakuta katika maeneo husika kwa kuwataka kuwa watulivu, huku akiahidi changamoto zinazokikabili chama hicho zitamalizika hivi karibuni.
Mbali na hilo pia aliwaahidi wanachama wa chama hicho kujiandaa ,kuchukua ofisi yao Buguruni muda wowote kuanzia sasa kwani wamefikia katika hatua nzuri.
Ziara hiyo ya kimya kimya imekuja siku chache baada ya Jeshi la Polisi kuzuia wanachama wa chama hicho, waliokuwa wamehamasishwa na Mbunge wa Temeke kwenda kufanya usafi katika ofisi za CUF Buguruni, Aprili 30, mwaka huu.
Hata hivyo, Jeshi la Polisi lilimzuia kwa Maalim Seif na wafuasi wake kufanya hivyo kwa maana ya kuweza kuhatarisha amani kwa wananchi iliyopo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu