Katibu tawala wa Mkoa wa Arusha asema serikali ina wajibu wa Kuhudumia watoto cha SOS.

In Kitaifa

Katibu tawala wa Mkoa wa Arusha Richard Kuitega amesema serikali ina wajibu wa kuanza kusaidia kituo cha Kuhudumia watoto cha SOS,ambacho kilikuwa kinahudumiwa na wafadhali kutoka nje ya nchi.

Akizungumza wakati alipotembelea taasisi inayohudumia watoto yatima ijulikanayo kama SOS children iliyopo Ngaramtoni mkoani Arusha  katibu huyo, amesema serikali ina Jukumu la kutoa ushirikiano ili kuweza kuendeleza miradi mbalimbali kwa manufaa ya Wananchi

Kuitega  amesema kuwa  serikali itaanza kwa kutoa wataalamu watakao toa huduma kituoni hapo  kama vile walimu ili kuhakikisha kuwa wanapunguza baadhi ya changamoto.

Kwa upande wake Mkurugenzi  wa Shirika hilo Fransis Msolo amesema kituo hicho kilikuwa chini ya wafadhili ,ambao kwa sasa wanajitoa hivyo ipo haja ya serikali kupandisha hadhi kituo hicho ili kiweze kutoa huduma ndani ya  Jamii.

Halikadhalika taasisi hiyo imeweza kutunza watoto Elfu moja 1000 ambapo wengine amefika  hadi elimu ya Juu ya Vyuo Vikuu na kuweza kujiendeleza Kimaisha.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu