Katibu tawala wa Mkoa wa Arusha asema serikali ina wajibu wa Kuhudumia watoto cha SOS.

In Kitaifa

Katibu tawala wa Mkoa wa Arusha Richard Kuitega amesema serikali ina wajibu wa kuanza kusaidia kituo cha Kuhudumia watoto cha SOS,ambacho kilikuwa kinahudumiwa na wafadhali kutoka nje ya nchi.

Akizungumza wakati alipotembelea taasisi inayohudumia watoto yatima ijulikanayo kama SOS children iliyopo Ngaramtoni mkoani Arusha  katibu huyo, amesema serikali ina Jukumu la kutoa ushirikiano ili kuweza kuendeleza miradi mbalimbali kwa manufaa ya Wananchi

Kuitega  amesema kuwa  serikali itaanza kwa kutoa wataalamu watakao toa huduma kituoni hapo  kama vile walimu ili kuhakikisha kuwa wanapunguza baadhi ya changamoto.

Kwa upande wake Mkurugenzi  wa Shirika hilo Fransis Msolo amesema kituo hicho kilikuwa chini ya wafadhili ,ambao kwa sasa wanajitoa hivyo ipo haja ya serikali kupandisha hadhi kituo hicho ili kiweze kutoa huduma ndani ya  Jamii.

Halikadhalika taasisi hiyo imeweza kutunza watoto Elfu moja 1000 ambapo wengine amefika  hadi elimu ya Juu ya Vyuo Vikuu na kuweza kujiendeleza Kimaisha.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu