Kenyatta asema ni haki yake kuikosoa mahakama.

In Kimataifa, Siasa

 

Rais Uhuru Kenyatta ametetea hatua yake ya kuikosoa mahakama ya juu na jaji mkuu David Maraga, kwa kubatilisha matokeo ya uchaguzi wa urais akisema ni haki yake kufanya hivyo.

Akizungumza katika kampeni za chama cha Jubilee eneo la Kajiado siku ya jana, Kenyatta amesisitiza madai yake kwamba mahakama hiyo ya juu ilipuuzilia mbali haki ya wananchi ili kumfurahisha mtu mmoja, aliyemtaja kuwa mpinzani wake Raila Odinga.

Amesema licha ya kuwa anaheshimu uamuzi wa mahakama hiyo, anajua kwamba alishinda uchaguzi huo kwa zaidi ya kura milioni 1.4.

Licha ya uamuzi huo Rais Kenyatta amesema kuwa ana imani atashinda tena uchaguzi huo wa marudio.

Insert 3-Kenyata

Kwa upande mwingine baada ya kiongozi wa upinzani Raila Odinga kutangaza kutoshiriki katika marudio ya Uchaguzi huo mpaka Tume ya Uchaguzi ifanyiwe mabadiliko.

Sasa habari mpya ni kuwa Tume hiyo imetangaza kundi la watu sita ambalo litasimamia uchaguzi huo.

Walioteuliwa ni Mkurugenzi Mkuu wa Tume hiyo Ezra Chiloba, Naibu wake Betty Nyabuto, Mkurugenzi wa Usajili wa wapiga kura pamoja na Mkuu wa Operesheni za Uchaguzi Immaculate Kasait, Naibu wake Mwaura Kamwati, Mkuu wa Operesheni za Tume na Mkuu wa Teknolojia James Muhati.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu