Kesi ya Aveva na Kaburu yapigwa kalendaa.

In Kitaifa

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imeahirisha kesi ya utakatishaji fedha ya USD 300,000, inayowakabili Rais wa klabu ya Simba Evans Aveva na Makamu wake Godfrey Nyange, hadi November 10 2017 kwa sababu upelelezi haujakamilika.
Wakili wa Serikali Vitalis Peter amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu Victoria Nongwa kuwa, kesi hiyo imeitishwa kwa ajili ya kutajwa na upelelezi haujakamilika, pia ameeleza uchunguzi wa kesi hiyo unaendelea na jalada la kesi bado lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).
Baada ya kueleza hayo Hakimu Nongwa ameahirisha kesi hiyo hadi November 10 2017, na watuhumiwa kurudishwa rumande.
Evans Elieza Aveva na makamu wake Geofrey, wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha fedha USD 300,000.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu