Kesi ya Aveva na Kaburu yapigwa kalendaa.

In Kitaifa

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imeahirisha kesi ya utakatishaji fedha ya USD 300,000, inayowakabili Rais wa klabu ya Simba Evans Aveva na Makamu wake Godfrey Nyange, hadi November 10 2017 kwa sababu upelelezi haujakamilika.
Wakili wa Serikali Vitalis Peter amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu Victoria Nongwa kuwa, kesi hiyo imeitishwa kwa ajili ya kutajwa na upelelezi haujakamilika, pia ameeleza uchunguzi wa kesi hiyo unaendelea na jalada la kesi bado lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).
Baada ya kueleza hayo Hakimu Nongwa ameahirisha kesi hiyo hadi November 10 2017, na watuhumiwa kurudishwa rumande.
Evans Elieza Aveva na makamu wake Geofrey, wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha fedha USD 300,000.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu