Kihamia awakilisha Jiji la Arusha Belgium.

In Kitaifa

WADAU mbalimbali  wa  Maendeleo  wamekutana katika Mkutano wa Maendeleo endelevu kwa viongozi wa  Majiji  kwa nchi za Afrika  Nchini Belgium ,ambapo  Tanzania imewakilishwa  na  Jiji la Arusha  chini ya Mkurugenzi  Athumani  Kihamia na ofisi ya  Jumuiya ya Ulaya Tanzania chini ya Afisa utekelezaji Anna Constantin  kutoka  Italy

Akizungumza na  redio 5 Mkurugenzi wa Jiji la Arusha  Athman Kihamia amesema  lengo  la Mkutano huo ni kuziwezesha  Serikali za Mitaa katika  Maendeleo, hasa  kilimo cha  Mazao  ya chakula.

Kihamia amesema mazao Mengi yamekuwa yakikosa namna bora ya uhifadhi haswa mazao ya Chakula hivyo kupitia Mkutano huo utawawezesha kutambua namna bora ya Utunzaji  ili yapate soko yakiwa yamechakatwa ili kuleta tija zaidi.

Aidha amesema kuwa nchi ya Tanzania inapendeza sana kwa kuwa,na  Sera nzuri na bora iliyopo Ya  Viwanda hasa vya Wakulima Wadogo.

 

Mkutano huo umeshirikisha mataifa  43 kutoka barani Afrika vikiwemo Vyuo vikuu mbalimbali vya kilimo sayansi na teknolojia vya Madrid,Palacky,Hague,Toulouse Capitole,  Antwelp  na  taasisi na mashirika mbalimbali ya maendeleo kama UNDP,EEAS, Kamisheni ya ulaya, wabunge wa jumuiya ya ulaya.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu