Kijana mdogo ameuawa nchini Venezuela katika siku nyingine ya maandamano dhidi ya Rais wa nchi hiyo Nicolas Maduro, maandamano ambayo kwa sasa yanazorotesha uchumi wa taifa hilo.

In Kimataifa

Kijana mdogo ameuawa nchini Venezuela katika siku nyingine ya maandamano dhidi ya Rais wa nchi hiyo Nicolas Maduro, maandamano ambayo kwa sasa yanazorotesha uchumi wa taifa hilo.

Kijana mwenye umri wa miaka 17, Luis Alviarez alipigwa risasi kifuani katika maandamano ya upinzani kwenye mji wa Guasimo, Mashariki mwa nchi hiyo.

Wito umetolewa wa kufanyika kwa uchunguzi kuhusu mazingira ya mauaji hayo.

 

Kiongozi wa wanafunzi mwenye umri wa miaka 22 Wilmer Arevalo naye yu mahututi baada ya kupigwa risasi kichwani kwenye maandamano mengine.

Pia kwenye jimbo la Tachira, wanaharakati wapinzani wa shirika la Foro penal wamesema zaidi ya watu 40 walikamatwa siku ya jumatatu .

Takriban watu 40 wameuawa tangu maandamano kuanza nchini humo majuma saba yaliyopita.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu