Kijana mdogo ameuawa nchini Venezuela katika siku nyingine ya maandamano dhidi ya Rais wa nchi hiyo Nicolas Maduro, maandamano ambayo kwa sasa yanazorotesha uchumi wa taifa hilo.

In Kimataifa

Kijana mdogo ameuawa nchini Venezuela katika siku nyingine ya maandamano dhidi ya Rais wa nchi hiyo Nicolas Maduro, maandamano ambayo kwa sasa yanazorotesha uchumi wa taifa hilo.

Kijana mwenye umri wa miaka 17, Luis Alviarez alipigwa risasi kifuani katika maandamano ya upinzani kwenye mji wa Guasimo, Mashariki mwa nchi hiyo.

Wito umetolewa wa kufanyika kwa uchunguzi kuhusu mazingira ya mauaji hayo.

 

Kiongozi wa wanafunzi mwenye umri wa miaka 22 Wilmer Arevalo naye yu mahututi baada ya kupigwa risasi kichwani kwenye maandamano mengine.

Pia kwenye jimbo la Tachira, wanaharakati wapinzani wa shirika la Foro penal wamesema zaidi ya watu 40 walikamatwa siku ya jumatatu .

Takriban watu 40 wameuawa tangu maandamano kuanza nchini humo majuma saba yaliyopita.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu