Kiungo wa Simba aingizwa mjini.

In Kitaifa, Michezo

Kiungo wa Simba Mghana James Kotei, amekaribishwa nchini Tanzania kwa kulizwa na wezi wa mitaa ya Msimbazi Kariakoo jijini Dar es salaam, kwa kuibiwa simu yake ya mkononi.

 

Kiungo huyo akiwa maeneo ya mitaa ya Msimbazi alijikuta akiingia mikononi mwa vibaka waliobobea kwa wizi, na kumuibia simu ya mkononi yenye thamani ya Sh milioni 1.4.

Simu hiyo alipewa zawadi na mmoja wa wanachama wa Simba, siku chache kabla ya mechi ya Ngao ya Jamii iliyoikutanisha Simba na Yanga kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.

Maelezo kutoka kwa mtu wa karibu wa klabu hiyo amedai kuwa, mchezaji huyo alistuka baada ya kufika makao makuu ya klabu hiyo mitaa ya Msimbazi akitokea Hotelini alikofikia na kujikuta hana simu.

Alipoulizwa Kotei kuhusiana na suala hilo amekiri wazi kuwa ni kweli amepatwa na balaa hilo, na kudai kuwa amepoteza mawasiliano yake muhimu.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu