Kiungo wa Simba aingizwa mjini.

In Kitaifa, Michezo

Kiungo wa Simba Mghana James Kotei, amekaribishwa nchini Tanzania kwa kulizwa na wezi wa mitaa ya Msimbazi Kariakoo jijini Dar es salaam, kwa kuibiwa simu yake ya mkononi.

 

Kiungo huyo akiwa maeneo ya mitaa ya Msimbazi alijikuta akiingia mikononi mwa vibaka waliobobea kwa wizi, na kumuibia simu ya mkononi yenye thamani ya Sh milioni 1.4.

Simu hiyo alipewa zawadi na mmoja wa wanachama wa Simba, siku chache kabla ya mechi ya Ngao ya Jamii iliyoikutanisha Simba na Yanga kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.

Maelezo kutoka kwa mtu wa karibu wa klabu hiyo amedai kuwa, mchezaji huyo alistuka baada ya kufika makao makuu ya klabu hiyo mitaa ya Msimbazi akitokea Hotelini alikofikia na kujikuta hana simu.

Alipoulizwa Kotei kuhusiana na suala hilo amekiri wazi kuwa ni kweli amepatwa na balaa hilo, na kudai kuwa amepoteza mawasiliano yake muhimu.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu