Baada ya kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Mwadui FC wakiwa ugenini, benchi la ufundi la Azam chini ya kocha wake mkuu, Aristica Cioaba raia wa Romania, limeweka bayana kwamba ni ngumu kupata matokeo mazuri wakiwa mkoani kutokana na wapinzani wao wengi kukamia michezo yao.
Azam ikiwa ugenini kwenye Uwanja wa Mwadui Complex mkoani Shinyanga, ililazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na wenyeji wao Mwadui wanaonolewa na kocha Jumanne Ntambi, kwa matokeo hayo Azam sasa wamefikisha pointi 12 baada ya mechi sita.
Mromania huyo amesema kuwa mchezo huo ulikuwa mgumu kwao licha ya kujiandaa vizuri kuibuka na ushindi lakini wapinzani wao waliwakomalia na kuambualia pointi moja pekee.
