Kongamano la kwanza la Shirika la Afya Duniani WHO kuhusu afya barani Afrika limemalizika jana

In Kimataifa

Kongamano la kwanza la Shirika la Afya Duniani WHO kuhusu afya barani Afrika limemalizika jana mjini Kigali, Rwanda, kwa kutoa ahadi ya kutimiza upatikanaji wa huduma za afya kwa wote barani humo.

Kongamano hilo la siku mbili lilikutanisha wajumbe zaidi ya 700 kutoka sekta mbalimbali ikiwemo wasomi, mawaziri wa afya, mashirika ya kiserikali na ya kijamii, na sekta binafsi.

Wajumbe hao walijadili masuala muhimu ikiwemo kutumia kupanua upatikanaji wa huduma za afya kwa wote kama njia kuu ya kutimiza malengo ya maendeleo endelevu kuhusu afya, ambayo yanahakikisha maisha bora na kuinua afya ya watu wote katika umri wote, na kuimarisha na kudumisha maendeleo ya nguvukazi kwenye sekta ya afya.

Wajumbe hao pia wametoa wito kwa serikali barani Afrika kuongoza na kusimamia vitendo vinavyolenga kujenga majukwaa ya uratibu na mfumo wa kanuni ili kutimiza upatikanaji wa huduma za afya, kuongeza uwekezaji wa ndani, na kusimamia na kutoa ripoti za maendeleo yanayopatikana.

 

 

 

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu