Kubenea atua Dodoma kuhojiwa.

In Kitaifa

Mbunge wa Ubungo kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Saed Kubenea amesafirishwa kwa ndege leo Jumatano asubuhi kwenda Dodoma anakohitajika mbele ya Kamati ya  Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.

Mbunge huyo jana Jumanne alisema alikuwa Kituo cha Polisi cha Oysterbay Wilayani Kinondoni akisubiri utaratibu wa safari hiyo ya kwenda kuhojiwa kama Spika wa Bunge Job Ndugai alivyoagiza.

Katibu wa wabunge wa Chadema, David Silinde akizungumzia safari ya mbunge huyo amesema, Kubenea amesafirishwa kwa ndege asubuhi kwenda Dodoma kwa ajili ya kuhojiwa na kamati ya Bunge.

Aidha, kwa upande Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema kuwa hana taarifa mpya lakini alitakiwa kuondoka leo asubuhi kwa ndege.

 

Hata hivyo, Kubenea amepelekwa mbele ya kamati ya Bunge akituhumiwa kwa taarifa alizozitoa kupitia mitandao ya kijamii kuwa Spika alisema uongo kuhusu idadi ya risasi alizopigwa Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu katika tukio lililotokea nyumbani kwake Area D mjini Dodoma Septemba 7

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu