Kubenea: Sihami CHADEMA

In Kitaifa, Siasa
Mbunge wa Jimbo la Ubungo kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, Said Kubenea amewataka wananchi wa jimbo lake na nchi nzima kwa ujumla kupuuzia taarifa zinazosambazwa dhidi yake kuhusu yeye kutaka kukihama chama chake.
Kebenea amesema kuwa ataendelea kuwa Mbunge wa jimbo la Ubungo na hana mpango wowote wa kuondoka CHADEMA kuhamia CCM.
“Wananchi wapuuze taarifa zozote zinazonihusisha mimi na kuondoka Chadema na kujiunga na CCM hizo ni za Uzushi mimi bado ni mwananchama wa Chadema na bado ni Mbunge wa Ubungo na sina mpango huo na sijawahi kuzungumza na mtu yoyote.” amesema Kubenea.
Kubenea ameyasema hayo baada ya kuibuka uvumi uliosambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii zikidai kuwa mbunge huyo anataka kuhamia CCM.
Hivi karibuni kumekuwa na vuguvugu kubwa la kisiasa ambapo wabunge pamoja na wanachama wa vyama mbalimbali wenye nyadhifa tofauti tofauti wakitangaza kujivua uanacham na kujiunga na chama kingine huku Chama Cha Mapinduzi CCM kikishuhudiwa kupata wafuasi wengi wanaokihamia.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu