Kundi la Boko Haram lapanga kulipua bomu katika mji mkuu wa Nigeria

In Kimataifa

Kundi la Boko Haram linapanga kulipua bomu katika mji mkuu wa Nigeria, Abuja, amesema mtu mmoja anayesemekana kuwa ni mpiganaji wa kundi hilo ,la wanamgambo wa itikadi kali za Kiislam, akizungumza katika  mkanda wa video ulionekana na shirika la habari la Reuters.

Mtu huyo amesema katika vidio hiyo kwamba, mashambulizi zaidi ya mabomu yanapangwa , ikiwa ni pamoja na mjini Abuja ambako wananachi ndipo wanapojihisi wapo salama.

Ukanda huo wa vidio umepatikana na waandishi habari wa tovuti ya habari ya Sahara iliyoko Marekani wakishirikiana na mwandishi habari wa nchini Nigeria Ahmad Salkida.

Shirika la habari la Reuters hata hivyo halikuweza mara moja kuthibitisha ukweli wa video hiyo.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu