Kunenge aibua kasoro machinjio ya kisasa.

In Kitaifa

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Aboubakar Kunenge ameonyesha kutoridhishwa na zoezi la majaribio ya uchinjaji wa Ng’ombe na Mbuzi kwenye machinjio ya kisasa Vingunguti baada ya kubaini kasoro za uendeshaji wa mtambo hiyo.

Miongoni mwa kasoro alizobaini RC Kunenge ni pamoja kukosekana kwa utaalamu wa uendeshaji wa mitambo, Zoezi la uchinjaji kutumia muda mrefu kuanzia hatua ya Kwanza Hadi mwisho, kukwamakwama kwa vifaa kwa baadhi ya maeneo, Kazi nyingi kufanywa na binadamu badala ya mashine Na wafanyakazi kufanya kazi kwa kubahatisha jambo lililopelekea Ng’ombe mmoja kutumia zaidi ya nusu saa Hadi kukamilika badala ya dakika 10.

Kutokana na hayo RC Kunenge amemtaka Mkandarasi wa ufungaji wa mashine, Mshauri wa Mradi, NHC na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala kufika ofisini kwake Alhamis ya Disemba 3 saa nne asubuhi.

Aidha RC Kunenge amewaelekeza NHC kuongeza kasi ili Ujenzi wa jengo ukamilike kwa wakati huku akimuelekeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala kuwa mkali.

Pamoja na hayo RC Kunenge amemtaka Mkandarasi wa ufungaji wa mitambo kuhakikisha anatoa elimu ya matumizi ya mitambo kwa wafanyakazi ili waweze kuzitumia.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu