Kwa mara ya kwanza shule ya sekondari ya Emboreet itaanza kuokea wanafunzi wa kidato cha tano kwa mwaka huu.

In Kitaifa

Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara ambayo haina shule ya kidato cha tano na sita, kwa mara ya kwanza shule ya sekondari ya Emboreet itaanza kupokea wanafunzi wa kidato cha tano kwa mwaka huu.

Mkuu wa wilaya ya Simanjiro mhandisi Zephania Chaula, akizungumza  kwenye kikao cha baraza la madiwani amesema wamejipanga shule hiyo ianze kupokea wanafunzi wa kidato cha tano, Julai mwaka huu.

Chaula amesema hadi hivi sasa shule ya sekondari Emboreet  ya kidato cha nne, imeboreshwa kwa ajili ya kupokea wanafunzi wa kidato cha tano, kwani awali wilaya ilikuwa haina shule ya kidato cha tano na sita.

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Jackson Sipiti eck, mkurugenzi mtendaji Yefred Myenzi na madiwani, wametenga sh 12 milioni, kwa ajili ya matengenezo ya miundombinu ya shule hiyo.

Amesema diwani wa kata ya Emboreet, Christopher Kuya anastahili kupongezwa, kwa kusimamia kitendo cha shule hiyo kufanikiwa kuwa na hatua ya kidato cha tano na sita kwani ni maendeleo kwa Simanjiro

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu