Kwa mara ya kwanza shule ya sekondari ya Emboreet itaanza kuokea wanafunzi wa kidato cha tano kwa mwaka huu.

In Kitaifa

Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara ambayo haina shule ya kidato cha tano na sita, kwa mara ya kwanza shule ya sekondari ya Emboreet itaanza kupokea wanafunzi wa kidato cha tano kwa mwaka huu.

Mkuu wa wilaya ya Simanjiro mhandisi Zephania Chaula, akizungumza  kwenye kikao cha baraza la madiwani amesema wamejipanga shule hiyo ianze kupokea wanafunzi wa kidato cha tano, Julai mwaka huu.

Chaula amesema hadi hivi sasa shule ya sekondari Emboreet  ya kidato cha nne, imeboreshwa kwa ajili ya kupokea wanafunzi wa kidato cha tano, kwani awali wilaya ilikuwa haina shule ya kidato cha tano na sita.

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Jackson Sipiti eck, mkurugenzi mtendaji Yefred Myenzi na madiwani, wametenga sh 12 milioni, kwa ajili ya matengenezo ya miundombinu ya shule hiyo.

Amesema diwani wa kata ya Emboreet, Christopher Kuya anastahili kupongezwa, kwa kusimamia kitendo cha shule hiyo kufanikiwa kuwa na hatua ya kidato cha tano na sita kwani ni maendeleo kwa Simanjiro

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu