Lissu apigwa Risasi.

In Kitaifa

Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA)na Rais wa Chama cha wanasheria Tanganyika (TLS) Tundu Lissu ameshambuliwa na risasi mchana huu.

Mbunge huyo kwa sasa anapatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa mkoani Dodoma

Mwanasiasa wa upinzani  Tundu Lissu ameripotiwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana jijini Dodoma.

Kwa mujibu wa taarifa ya chama kikuu cha upinzani CHADEMA kwa vyombo vya habari, tukio hilo limetokea wakati mbunge huyo akiwa nyumbani kwake.

Chama hicho kimelaani vikali tukio hilo.

Kamanda wa polisi mkoani Dodoma, Kamishna Msaidizi , Jires Mroto amesema   wameanza uchunguzi wa tukio hilo.

“Tunaomba wananchi wenye taarifa ya uhalifu huu, waweze kujitokeza” amesema Kamanda Mroto.

Taarifa zaidi zitakuijia.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu