Liverpool yatupwa nje michuano ya Carabao.

In Kimataifa, Michezo

 

Nchini Uingereza michuano ya Carabao Cup imeanza vibaya kwa majogoo wa London Liverpool baada ya kukubali kipigo kutoka kwa Leicester City katika mchezo uliopigwa katika uwanja wa King Power.

Mshambuliaji Shinji Okazaki alitangulia kuipatia Leicester City katika dakika ya 65 likiwa ni bao lake la nne kuifungia Leicester msimu huu kabla ya Islam Slimani kupachika bao la pili kwa shuti kali na kuiondosha Liverpool katika michuano ya Carabao Cup kwa ushindi wa 2-0.

Kwingineko bao pekee lililofungwa na Delle Ali limeifanya Tottenham kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Burnley  huku Swansea City wakipata ushindi wa mabao 2 ugenini dhidi ya Reading.

Michuano hiyo itaendelea leo katika raundi ya tatu ambapo michezo michezo mitano itapigwa leo katika viwanja tofauti.

Arsenal watacheza dhidi ya Doncaster, Chelsea watacheza na Nottingham Forest,Everton dhidi ya Sunderland, Manchester United dhidi ya Burton Albion wakati West Bromwich watakipiga didi ya Man City.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu