Luanda waupiku Mji wa Hong Kong kua mji ulio ghali zaidi kwa wafanyakazi wataalamu duniani.

In Kimataifa

Mji mkuu wa Angola , Luanda umeupiku mji wa Hong Kong na kuwa nafasi ya kwanza ya mji ulio ghali zaidi wa maisha kwa wafanyakazi wataalamu duniani.

Kulingana na uchunguzi wa kila mwaka unaorodhesha viwango vya ughali wa maisha kwa wafanyakazi wataalamu katika miji ya dunia, malipo ya nyumba ya vyumba viwili vya kiwango cha wataalamu mjini Luanda ni dola 4,800 za Kimarekani kwa mwezi, wakati kitafunio cha Hamburger mkahawani ni dola 11 na nusu.

Uchunguzi huo umegundua mji wenye maisha yalio rahisi kwa wafanyakazi wa kigeni ni Tunis nchini Tunisia ukishika nafasi ya 209 na kufuatiwa na mji mkuu wa Kardztan -Bishkek na Skopye Macedonia.

Ni mara ya pili katika kipindi cha miaka mitatu, Luanda unatajwa kuwa mji ghali kabisa kimaisha kuanzia nyumba , usafiri na mavazi , katika orodha ya miji 209 duniani.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu