Luhaga Mpina ameviagiza vyombo vya dola kuwakamata mawakala wa pamba.

In Kitaifa

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. Luhaga Mpina ameviagiza vyombo vya dola kuwakamata na kuwashitaki mahakamani mawakala wa makampuni ya ununuzi wa zao la Pamba katika mikoa 15 ya kanda ya magharibi wanaowasambazia wakulima viuatilifu vilivyokwisha muda wake wa matumizi.

Mh. Mpina, ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Kisesa katika wilaya ya Meatu mkoani Simiyu, akizungumza na wakulima wa pamba wa vijiji vinne vya kata ya Mwabusalu ambavyo vinatekeleza mradi wa uzalishaji wa mbegu bora ya UKM08, amepiga marufuku tabia ya baadhi ya wakulima kuchanganya mazao mengine kama mahindi na mimea jamii ya mikunde kwenye shamba la pamba.

Hata Akiwa katika kiwanda cha kuchambua pamba kilichojengwa na mwekezaji kampuni ya Gaki Investment tangu mwaka 2012 bila kufanya kazi na hivyo kuminya fursa za ajira kwa wananchi wa jimbo la Kisesa.

Wakulima wa vijiji vya Mwabusalu, Mwakipugila, Ikigijo na Nzanza wamefanikiwa kuzalisha kilo 500 hadi 700 kwa ekari moja kwa kutumia mbegu za UKM08, ukilinganisha na mbegu zilizotumika msimu uliopita wa 2014/2015 za UK91 iliyokuwa ikizalisha wastani wa kilo 200 hadi 300 kwa ekari moja.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu