Lukaku alinipiga teke usoni kwa makusudi…

In Kimataifa, Michezo

Beki wa Liverpool Dejan Lovren amemshutumu mshambuliaji wa Manchester United Romelu Lukaku kwa kumpiga teke usoni kwa makusudi katika mechi ya Jumamosi.
Wawili hao walihusika katika mgogoro wa muda mfupi kabla ya kukamilika kwa kipindi cha kwanza katika mechi iliotoka sare ya 0-0 katika uwanja wa Anfield, huku Lovren akisalia amejibiringisha katika uwanja akishikilia uso wake kwa uchungu mwingi.
Mkufunzi wa Liverpool Jurgen Klopp alisema kuwa alidhani kwamba Lukaku alihitaji kupewa kadi nyekundu , lakini hakuna hatua yoyote iliochukuliwa.
”Ukweli ni kwamba alifanya alichokifanya kwa makusudi”, alisema Lovren.”Alikuwa juu yangu na angeondoka tu”.
”Kawaida akifanya hivyo yeye huomba msamaha , lakini nilimuona akiwa amekasirika wakati wa mechi kwa hivyo pengine hiyo ilikuwa sababu”.
Alipoulizwa iwapo hakufurahia kwamba mshambuliaji huyo wa Ubelgiji hatopewa adhabu yoyote , Lovren alijibu.”Huo sio uamuzi wangusiwezi kusema sikufurahia lakini hivyo ndivyo ilivyo”.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu