Shukurani kwake, mshambuliaji mpya, Ibrahim Hajib Migomba aliyefunga bao hilo pekee kipindi cha kwanza na sasa Yanga inafikisha pointi nne baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Lipuli ya Iringa kwenye mchezo wa kwanza nyumbani, Dar es Salaam.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Suleiman Kinugani wa Morogoro, aliyesaidiwa na Khalfan Sika wa Pwani na Hajji Mwalukuta wa Tanga, Hajib alifunga bao hilo dakika ya 16 kwa shuti la umbali wa mita 30 la mpira wa adhabu, baada ya yeye mwenyewe kuangushwa.
Kocha wa Yanga, George Lwandamina amesema timu yake haikucheza vizuri jana Njombe kwa sababu Uwanja mbaya na baridi kali
Na baada ya mchezo huo, Lwandamina leo amesema kwamba hawakucheza katika kiwango chao kutokana na mazingira ya Uwanja na hali ya hewa, lakini wanashukuru wamechukua pointi tatu.
“Ninamshukuru Mungu tumeshinda, lakini ulikuwa mchezo mgumu sana kutokana na mazingira magumu ya Uwanja wa na hali ya hewa,”alisema.