Maafisa usalama Somalia wafukuzwa kazi.

In Kimataifa

Serikali ya Somalia imewafuta kazi maafisa wawili wa usalama wa ngazi za juu, kufuatia shambulio la mabomu yaliyosababisha mauaji ya watu 27 Jumamosi iliyopita jijini Mogadishu.

Shambulio hilo inaripotiwa kuwa lilitekelezwa na kundi la kigaidi la Al -Shabaab.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini humo Abdihakin Dahir Saiid na Mkurugenzi wa Intelijensia Abdillahi Mohamed Sanbaloosh, ndio waliokubwa na adhabu hiyo saa chache baada ya tukio hilo la kigaidi.

Tukio hilo la Jumamosi limeripotiwa ikiwa ni wiki mbili tangu litokee shambulio lingine kubwa zaidi la kigaidi, lililosababisha vifo vya watu 358.

Hata hivyo kundi la Al-Shabaab ambalo linaushirika na kundi la Al-Qaeda, limekanusha kuhusika na tukio la awali huku likikiri kuhusika na tukio la Jumamosi iliyopita

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu