Maafisa usalama Somalia wafukuzwa kazi.

In Kimataifa

Serikali ya Somalia imewafuta kazi maafisa wawili wa usalama wa ngazi za juu, kufuatia shambulio la mabomu yaliyosababisha mauaji ya watu 27 Jumamosi iliyopita jijini Mogadishu.

Shambulio hilo inaripotiwa kuwa lilitekelezwa na kundi la kigaidi la Al -Shabaab.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini humo Abdihakin Dahir Saiid na Mkurugenzi wa Intelijensia Abdillahi Mohamed Sanbaloosh, ndio waliokubwa na adhabu hiyo saa chache baada ya tukio hilo la kigaidi.

Tukio hilo la Jumamosi limeripotiwa ikiwa ni wiki mbili tangu litokee shambulio lingine kubwa zaidi la kigaidi, lililosababisha vifo vya watu 358.

Hata hivyo kundi la Al-Shabaab ambalo linaushirika na kundi la Al-Qaeda, limekanusha kuhusika na tukio la awali huku likikiri kuhusika na tukio la Jumamosi iliyopita

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu