Maandamano makubwa yafanyika katika miji mbalimbali nchini Ufaransa kushinikiza serikali kuboresha maslahi ya wafanyakazi.

Nchini Ufaransa, kumekuwa na maandamano makubwa katika miji mbalimbali nchini humo kuishinikiza serikali kuboresha maslahi ya wafanyikazi.

Ufaransa inasema wanajeshi wake wamewauawa na kuwakamata zaidi ya waasi 20 katika mpaka wa Mali na Burkina Faso.

Jeshi nchini humo linasema kuwa liliwashambulia waasi hao kwa mashambulizi ya angaa lakini haijafahamika walikuwa ni waasi gani.

Hatua hii imekuja baada ya kuuawa kwa mwanajeshi wa Ufaransa katika eneo hilo mwezi Aprili.

Mali imeendelea kukabiliwa na waasi na mwaka 2013, iliomba msaada wa jeshi la Ufaransa ambalo limekuwa likifanya msako na kusaidia mapambana na waasi hao.

Mashambulizi haya yamekuja baada ya bunge la Mali mwishoni mwa wili iliyopita, kupitisha mswada wa kuendelea kuwepo kwa hali ya hatari Kaskazini mwa nchi hiyo kwa sababu za kiusalama.

Ufaransa imetuma wanajeshi wake 4000 kupambana na waasi Kaskazini mwa Mali.

Exit mobile version