Maas asema janga la COVID-19 limedhoofisha Haki za Binadamu duniani.

In Kimataifa

Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Ujerumani Heiko Maas amesema leo kuwa janga la virusi vya corona limesababisha kuanguka kwa hali ya Haki za Binadamu duniani .

Akizungumza wakati wa mjadala ndani ya bunge la shirikisho mjini Berlin, Maas amesema ulimwengu unashuhudia jinsi mzozo wa COVID-19 unavyowaimarisha watawala wanaotumia mabavu.

Maas ameorodhesha hatua za ukandamizaji zilizochukuliwa dhidi ya waandishi habari nchini Urusi, Venezuela, Iran, Uturuki na China kama mifano ya matumizi ya nguvu katika kushughulikia kadhia ya Corona.

Mwanasiasa huyo wa chama cha SPD pia amegusia namna baadhi ya mataifa ya Ulaya ikiwemo Hungary yanavyotumia vizuizi vya kukabiliana na virusi vya corona kudhoofisha utawala wa sheria.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu