MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

In Kimataifa

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo la kusini mwa Afrika kwa mara ya pili ndani ya mwezi mmoja.

Kiasi cha kutisha cha maji ya kahawia yametiririka katika vitongoji, na kusomba nyumba.

Kitovu cha kibiashara cha Malawi, Blantyre, kimerekodi vifo vingi, 158, wakiwemo 36 katika maeneo ya maporomoko ya ardhi.

Serikali imetangaza hali ya janga katika wilaya 10 za kusini ambazo zimeathiriwa zaidi na dhoruba hiyo.

Wafanyakazi wa uokoaji wamezidiwa, na wanatumia majembe kujaribu kuwatafuta manusura waliofukiwa na udongo.

Shirika la serikali la kusaidia majanga limesema idadi ya waliofariki imeongezeka kutoka 99 siku ya Jumatatu hadi 190, huku takriban watu 584 wakijeruhiwa na 37 bado hawajulikani walipo.

Zaidi ya watu 20,00 wamekimbia makazi yao, iliongeza.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu