MAGUFULI:Walarushwa wafungwe

In Kitaifa

Rais Dkt. John Magufuli, amesema anataka wala rushwa wengi wafungwe licha ya kuwa, kuna baadhi ya watu hawataki kusikia kauli hiyo.

Hayo yamesema  Ikulu Dar es Salaam baada ya kumwapisha Naibu Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Brigedia Jenerali John Mbungo.

Amesema wakifungwa wala rushwa nchi haitakuwa na rushwa kwani  ndio wamekuwa walimu wa walarushwa nchini,huku akiwataka viongozi hao wa Takukuru kwenda kusimamia kazi hiyo na wasimwogope mtu yeyote.

Rais Magufuli ameeleza kutoridhishwa na taratibu za uchunguzi na uendeshaji wa mashtaka ya rushwa yanavyochukua muda mrefu, na ametoa wito kwa viongozi wa Takukuru kufanyia kazi eneo hilo ili vita dhidi ya rushwa ionekane ikizaa matunda haraka.

Aidha amewataka viongozi wote nchini kushirikiana katika jukumu la mapambano dhidi ya rushwa ili kuepusha madhara ya tatizo hilo katika uchumi na ustawi wa jamii.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu