MAGUFULI:Walarushwa wafungwe

Rais Dkt. John Magufuli, amesema anataka wala rushwa wengi wafungwe licha ya kuwa, kuna baadhi ya watu hawataki kusikia kauli hiyo.

Hayo yamesema  Ikulu Dar es Salaam baada ya kumwapisha Naibu Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Brigedia Jenerali John Mbungo.

Amesema wakifungwa wala rushwa nchi haitakuwa na rushwa kwani  ndio wamekuwa walimu wa walarushwa nchini,huku akiwataka viongozi hao wa Takukuru kwenda kusimamia kazi hiyo na wasimwogope mtu yeyote.

Rais Magufuli ameeleza kutoridhishwa na taratibu za uchunguzi na uendeshaji wa mashtaka ya rushwa yanavyochukua muda mrefu, na ametoa wito kwa viongozi wa Takukuru kufanyia kazi eneo hilo ili vita dhidi ya rushwa ionekane ikizaa matunda haraka.

Aidha amewataka viongozi wote nchini kushirikiana katika jukumu la mapambano dhidi ya rushwa ili kuepusha madhara ya tatizo hilo katika uchumi na ustawi wa jamii.

Exit mobile version