Mahakama ya hakimu mkazi ya wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma imemuhukumu kifungo cha maisha kijana mmoja aliye fahamika kwa jina la Peter Semango almaarufu Madinda mwenye umri wa miaka 23 mkazi wa Kimagai kwa kosa la kumbaka na kumlawiti mdogo wake wa kike mwenye umri wa miaka 8.

In Kitaifa
Mahakama  ya hakimu mkazi ya wilayani  Mpwapwa mkoani Dodoma imemuhukumu kifungo cha maisha kijana mmoja aliye fahamika kwa jina la Peter Semango almaarufu Madinda mwenye umri wa miaka 23 mkazi wa Kimagai kwa kosa la kumbaka na kumlawiti mdogo wake wa kike mwenye umri wa miaka 8.
Hukumu hiyo imetolewa jana na Hakimu mkazi wa Mahakama hiyo,PASCHAL MAYUMBA baada ya mahakama kujiridhisha bila kuacha shaka lolote kuhusiana na tukio hilo.
Kesi hiyo ilivuta hisia za wasikilizaji na wanaharakati wa haki za mtoto katika Mahakama hiyo.
Akimsomea shitaka hilo  mwendesha mashitaka wa polisi GOOD WILL IKEMA amesema mtuhumiwa huyo Alitenda kosa hilo mnamo Juni 13mwaka huu nyumbani kwao mnamo majira ya saa 4 usiku baada ya kumvizia akiwa amelala.
Mwendesha mashitaka huyo amebainisha kuwa kutokana na kijana huyo kufanya kitendo hicho cha ubakaji na ulawiti kwa mdogo wake hivyo anakabiliwa na makosa hayo kinyume na kifungu namba 130kifungu kidogo cha kwanza na cha pili (1 nakifungu cha 131ya kanuni ya adhabu iliyo fanyiwa marejeo mwaka 2002.
Hata hivyo GOODWILL aliiomba Mahakama itoe adhabu kali dhidi ya kijana huyo ili iwe fundisho kwa wengine.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu