Mahakama ya Rufaa nchini Kenya imebatilisha uamuzi wa Mahakama Kuu uliokuwa umefuta kandarasi ya kupiga chapa karatasi za kura za urais.

In Kimataifa

Mahakama ya Rufaa nchini Kenya imebatilisha uamuzi wa Mahakama Kuu uliokuwa umefuta kandarasi ya kupiga chapa karatasi za kura za urais kufuatia kesi iliyokuwa imewasilishwa na muungano wa upinzani.

Majaji wa mahakama ya rufaa wamesema mahakama hiyo ya chini ilikosea ilipoamua kwamba wananchi walifaa kushirikishwa katika uamuzi wa kutoa kandarasi hiyo ya thamani ya $24m (£18m) kwa kampuni ya Al Ghurair kutoka Dubai.

Mahakama hiyo imesema si lazima kwa taasisi ya serikali inapoamua kutoa zabuni moja kwa moja kushirikisha wananchi katika kufanya uamuzi au hata kufikia uamuzi wenyewe wa kutumia njia hiyo kutoa kandarasi hiyo.

Aidha, majaji hao wamesema mahakama ilifaa kuzingatia maslahi ya wananchi na haki yao ya kushiriki katika uchaguzi huru na wa haki.

Wamesema ni lazima uchaguzi mkuu ufanyike tarehe 8 Agosti na majaji wa Mahakama Kuu walifaa kuzingatia muda uliopo kwa Tume ya Uchaguzi (IEBC) kujiandaa ili kufanikisha uchaguzi huo.

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu