Mahakama yaondoa marufuku ya maandamano Kenya.

In Kimataifa

Mahakama kuu nchini kenya imeondoa kwa muda marufuku kwa maandamano dhidi ya tume ya uchaguzi ya chi hiyo IEBC.
Muungano wa upinzani (Nasa) ulikuwa tayari umetangaza kuwa hingefanya maandamano leo dhidi ya tume ya uchaguzi, ili kuwaruhusu viongozi wake kuwatembelea watu walipigwa na polisi wakati wa maandamano.
Katika taarifa, msemaji wa kiongozi wa Nasa, Raila Odinga, Dennis Onyango, alisema kuwa watasitisha maandamano leo kuonyesha huruma kwa wale waliojeruhiwa na polisi wakati wa maandamano.
Nasa imewalaumu polisi kwa kutumia nguvu nyingi dhidi ya waandamanaji, madai ambao polisi wamekana.
Mwanafunzi aliuawa kwa kupigwa risasi siku ya Jumatatu wakati wa maandamano mjini Kisumu, magharibi mwa Kenya.
Maandamano yalizuka baada ya uchaguzi wa mwezi Agosti, ulioshindwa na Rais Uhuru Kenyatta.
Mahakama ya juu zaidi iliamua kuwa uchaguzi huo ulikuwa na hitilafu.
Bw. Odinga anasema hatashiriki marudio ya uchaguzi wa wiki ijayo kwa sababu matakwa yake kwa tume ya uchaguzi kufanyiwa mabadiliko hayajatekelezwa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu