Mahakama yaondoa marufuku ya maandamano Kenya.

In Kimataifa

Mahakama kuu nchini kenya imeondoa kwa muda marufuku kwa maandamano dhidi ya tume ya uchaguzi ya chi hiyo IEBC.
Muungano wa upinzani (Nasa) ulikuwa tayari umetangaza kuwa hingefanya maandamano leo dhidi ya tume ya uchaguzi, ili kuwaruhusu viongozi wake kuwatembelea watu walipigwa na polisi wakati wa maandamano.
Katika taarifa, msemaji wa kiongozi wa Nasa, Raila Odinga, Dennis Onyango, alisema kuwa watasitisha maandamano leo kuonyesha huruma kwa wale waliojeruhiwa na polisi wakati wa maandamano.
Nasa imewalaumu polisi kwa kutumia nguvu nyingi dhidi ya waandamanaji, madai ambao polisi wamekana.
Mwanafunzi aliuawa kwa kupigwa risasi siku ya Jumatatu wakati wa maandamano mjini Kisumu, magharibi mwa Kenya.
Maandamano yalizuka baada ya uchaguzi wa mwezi Agosti, ulioshindwa na Rais Uhuru Kenyatta.
Mahakama ya juu zaidi iliamua kuwa uchaguzi huo ulikuwa na hitilafu.
Bw. Odinga anasema hatashiriki marudio ya uchaguzi wa wiki ijayo kwa sababu matakwa yake kwa tume ya uchaguzi kufanyiwa mabadiliko hayajatekelezwa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu