Majaji wa Mahakama ya Juu Kenya wameanza kuandika uamuzi.

In Kimataifa, Siasa

Majaji wa Mahakama ya Juu wameanza kuandika uamuzi wa kesi ya kupinga ushindi wa rais Uhuru Kenyatta, iliyowasilishwa na kiongozi wa Muungano wa upinzani NASA Raila Odinga.

Hatua hii inakuja baada ya Majaji hao kutamatisha kibarua cha kusikiliza Mawakili wa upande wa Tume ya uchaguzi, wale wanaomwakilisha rais Kenyatta na wale wa muungano wa upinzani NASA.

Mawakili wa NASA, wakiongozwa na James Orengo, wanataka Mahakama hiyo kutupilia mbali kesi hiyo baada ya kuonesha kuwa kulikuwa na ushahidi mkubwa, Uchaguzi huo haukuwa huru na haki.

Akitoa ripoti ya mwisho, Orengo alisema ikiwa Mahakama hiyo itaangalia kikamilifu ushahidi wote uliowasilishwa, basi ushindi huo utatupiliwa mbali.

Paul Muite anayewakilisha Tume ya Uchaguzi katika kesi hiyo alisema kuwa, pamoja na kwamba huenda kulikuwa na dosari ndogondogo, zoezi hilo lilikwenda vizuri.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu