Majaliwa ataka vyombo vya dola vipewe muda wa uchunguzi.

In Kitaifa

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema kuwa vyombo vya dola vinatakiwa kupewa muda kwaajili ya kufanya uchunguzi katika matukio mbalimbali ya mashambulizi dhidi ya wananchi na viongozi.

Ameyasema hayo hii leo Bungeni Mjini Dodoma, wakati wa maswali na majibu mara baada ya kuulizwa swali na kiongozi wa kambi rasmi bungeni, Freeman Mbowe kuhusu kurusu vyombo vya kimataifa kufanya uchunguzi wa tukio la kushambuliwa kwa mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu

“Suala hili la kushambuliwa kwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ni muendelezo wa matukio ambayo yamekuwa yakitokea sehemu mbalimbali nchini, ikiwemo mkoa wa Pwani katika Wilaya za Mkuranga, Rufiji na Kibiti, hivyo, vyombo vya dola vipewe muda wa uchunguzi ili kuwabaini waharifu,”amesema Majaliwa

Hata hivyo, ameongeza kuwa Tundu Lissu ni mbunge mwenzao hivyo suala hilo linamhusu kila mbunge wa kutoka upande wowote, hivyo linashughulikiwa kama matukio mengine yanavyoshughulikiwa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu