Majaliwa ataka vyombo vya dola vipewe muda wa uchunguzi.

In Kitaifa

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema kuwa vyombo vya dola vinatakiwa kupewa muda kwaajili ya kufanya uchunguzi katika matukio mbalimbali ya mashambulizi dhidi ya wananchi na viongozi.

Ameyasema hayo hii leo Bungeni Mjini Dodoma, wakati wa maswali na majibu mara baada ya kuulizwa swali na kiongozi wa kambi rasmi bungeni, Freeman Mbowe kuhusu kurusu vyombo vya kimataifa kufanya uchunguzi wa tukio la kushambuliwa kwa mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu

“Suala hili la kushambuliwa kwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ni muendelezo wa matukio ambayo yamekuwa yakitokea sehemu mbalimbali nchini, ikiwemo mkoa wa Pwani katika Wilaya za Mkuranga, Rufiji na Kibiti, hivyo, vyombo vya dola vipewe muda wa uchunguzi ili kuwabaini waharifu,”amesema Majaliwa

Hata hivyo, ameongeza kuwa Tundu Lissu ni mbunge mwenzao hivyo suala hilo linamhusu kila mbunge wa kutoka upande wowote, hivyo linashughulikiwa kama matukio mengine yanavyoshughulikiwa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu