Makamu wa Rais asema Taifa halipo tayari kupokea misaada isiyoendana na Mila na Desturi.

In Kitaifa

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan, amesema Taifa halipo tayari hata kidogo kupokea misaada yenye masharti ambayo haiendani na mila na desturi za Kitanzania.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Rais Mstaafu wa Ireland Mary Robinson pamoja na Mwanzilishi wa Taasisi ya Graca Machel, Craca Machel pamoja na ujumbe walioambatana nao Ikulu­ Jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema kuwa kuna baadhi ya wafadhili wanaisaidia Serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na bila masharti mabaya lakini kuna baadhi ya wafadhili wanaonyesha wazi kuwawanataka Serikali ikubali masharti yao.

Amesema kutokana na changamoto hiyo Serikali itaendelea kusimamia maadili ya Taifa ipasavyo na imeweka mipango na mikakati mizuri kwa ajili ya kuongeza mapato yake ya ndani ili kuondokana na utegemezi kutoka kwa baadhi ya wafadhili ambao wanaahidi kuchangia bajeti kuu ya Serikali lakini mwisho hawafanyi hivyo.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu