Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesema kamwe Serikali haitagawa chakula, kwa wananchi wavivu ambao hawataki kufanya kazi na kusubiri chakula kutoka serikalini.

In Kitaifa

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesema kamwe Serikali haitagawa chakula, kwa wananchi wavivu ambao hawataki kufanya kazi na kusubiri chakula kutoka serikalini.

Ametoa kauli hiyo wakati akihutubia mamia ya wananchi wa Manispaa ya Musoma ,katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Mukendo mjini humo.

Samia amesisitiza kuwa Serikali itapeleka chakula kwa wananchi ambao mazao yao yaliharibiwa kwa mvua, au yalikauka kwa ukame au kwa maafa mengine ,na sio kwa wananchi wanaokaa vijiweni mchana kutwa bila kufanya kazi wakisubiri neema ya chakula kutoka kwa Serikali.

Amewahimiza wananchi kote nchini kuendelea kufanya kwa bidii ikiwemo shughuli za kilimo, na pindi wanapovuka wajiwekee akiba na waache tabia ya kuuza mazao yote wanayovuna, ili kukabiliana na tatizo la uhaba wa chakula kwenye familia zao.

Pia aliwataka viongozi wa mkoa wa Mara washirikiane na wananchi katika kuwaelemisha mbinu bora za kilimo ili waweze kupata mazao mengi ikilinganishwa na hali ilivyo kwa sasa.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu