Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesema kamwe Serikali haitagawa chakula, kwa wananchi wavivu ambao hawataki kufanya kazi na kusubiri chakula kutoka serikalini.

In Kitaifa

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesema kamwe Serikali haitagawa chakula, kwa wananchi wavivu ambao hawataki kufanya kazi na kusubiri chakula kutoka serikalini.

Ametoa kauli hiyo wakati akihutubia mamia ya wananchi wa Manispaa ya Musoma ,katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Mukendo mjini humo.

Samia amesisitiza kuwa Serikali itapeleka chakula kwa wananchi ambao mazao yao yaliharibiwa kwa mvua, au yalikauka kwa ukame au kwa maafa mengine ,na sio kwa wananchi wanaokaa vijiweni mchana kutwa bila kufanya kazi wakisubiri neema ya chakula kutoka kwa Serikali.

Amewahimiza wananchi kote nchini kuendelea kufanya kwa bidii ikiwemo shughuli za kilimo, na pindi wanapovuka wajiwekee akiba na waache tabia ya kuuza mazao yote wanayovuna, ili kukabiliana na tatizo la uhaba wa chakula kwenye familia zao.

Pia aliwataka viongozi wa mkoa wa Mara washirikiane na wananchi katika kuwaelemisha mbinu bora za kilimo ili waweze kupata mazao mengi ikilinganishwa na hali ilivyo kwa sasa.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu