Makamu wa rais wa Zimbabwe aliyefutwa kazi atoroka.

In Kimataifa

Aliyekuwa makamu wa rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa ambaye alifutwa kazi siku ya Jumatatu amelitoroka taifa hilo kufuatia vitisho vya kifo , kulingana na washirika wake.

Rais Mugabe mwenye umri wa miaka 93 amemshtumu aliyekuwa makamu wake kwa kupanga njama za kuchukua mamlaka kutoka kwake.

”Alienda katika kanisa moja na Apostolic kujua ni lini Mugabe atafariki. Lakini aliambia kwamba atafariki wa kwanza” , Mugabe aliwaambia wafuasi wake sikju ya Jumatano.

Mke wa rais Grace Mugabe sasa ndio aliye kifua mbele kumrithi rais mumewe.

Bi Mugabe amekuwa akipigania kung’atuliwa kwa makamu huyo katika mkutano maalum wa chama tawala cha Zanu-PF mwezi Ujao.

Chama cha Zanu PF kilimfurusha Mnangagwa katika chama hicho siku ya Jumatano.

Bwana Mugabe alimtaja naibu wake wa zamani kuwa miongoni mwa waliopanga njama na akaonya kuwa atawachukulia hatua maafisa wengine wa chama hicho walioshirikiana na Mnangagwa.

”Tulimjua kitambo bwana Mnangagwa .Lakini hatukutaka kuwalezea. Alidhani kwamba kwa kuwa mwandani wangu nitambeba na kumpatia urais. Lakini sikufariki, na sikujiuzulu”, aliwaambaia wafuasi wake katika makao makuu ya chama cha Zanu PF mjini Harare.

”Tunatumai tutakabiliana na wengine ambao pia walikuwa na njama kama hiyo” , aliongezea.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu