Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ametoa onyo
kwaa maafisa usalama barabarani wanaoendelea kuwakamata
waendesha pikipiki maarufu kama Bodaboda pamoja na bajaji
ambao katika kipindi hiki cha mlipuko wa virusi vya Corona
wameruhusiwa kuingia katika ya jiji kinyume na ilivyokuwa
awali.
RC Makonda pia amewaomba madereva daladala kuwapakiza
wanafunzi kwani tayari shule zimefunguliwa kwa kidato cha sita
na vyuo, hivyo kuwapakiza katika daladala zao wanafunzi
wasiopungua wanne.