Malori 600 ya Tanzania yakamatwa Zambia.

In Kimataifa

Maafisa nchini Tanzania wanasema kuwa wanatafuta suluhu ya kidiplomasia kuhusu kisa kinachohusisha Zambia, ambapo malori 600 ya Tanzania yamekamatwa na kuzuiliwa kwa kipindi cha miezi miwili.

Zambia iliyakamata malori hayo yalipokuwa yakirudi kutoka DR Congo ambapo yalikuwa yameenda kubeba mbao.

Rais wa Zambia Edgar Lungu siku ya Jumatatu alisema kuwa hatokubali taifa lake kutumika kama kituo cha miti ya mbao akidai kuwa madereva wa malori kutoka Tanzania wanakiuka sheria kuhusu usafirishaji mbao.

Maafisa wa Tanzania wametoa wito kwa maafisa wao katika ubalozi wao nchini Zambia kuwasilisha swala hilo na maafisa husika ili kupata suluhu ya haraka.

Muungano wa madereva wa malori wa Tanzania Tatao umesema kuwa wanachama wake walifuata maelezo yote kuhusu ununuzi na mauzo ya nje ili kuweza kuingia nchini DR Congo.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu