Malori 600 ya Tanzania yakamatwa Zambia.

In Kimataifa

Maafisa nchini Tanzania wanasema kuwa wanatafuta suluhu ya kidiplomasia kuhusu kisa kinachohusisha Zambia, ambapo malori 600 ya Tanzania yamekamatwa na kuzuiliwa kwa kipindi cha miezi miwili.

Zambia iliyakamata malori hayo yalipokuwa yakirudi kutoka DR Congo ambapo yalikuwa yameenda kubeba mbao.

Rais wa Zambia Edgar Lungu siku ya Jumatatu alisema kuwa hatokubali taifa lake kutumika kama kituo cha miti ya mbao akidai kuwa madereva wa malori kutoka Tanzania wanakiuka sheria kuhusu usafirishaji mbao.

Maafisa wa Tanzania wametoa wito kwa maafisa wao katika ubalozi wao nchini Zambia kuwasilisha swala hilo na maafisa husika ili kupata suluhu ya haraka.

Muungano wa madereva wa malori wa Tanzania Tatao umesema kuwa wanachama wake walifuata maelezo yote kuhusu ununuzi na mauzo ya nje ili kuweza kuingia nchini DR Congo.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu