Malori 600 ya Tanzania yakamatwa Zambia.

In Kimataifa

Maafisa nchini Tanzania wanasema kuwa wanatafuta suluhu ya kidiplomasia kuhusu kisa kinachohusisha Zambia, ambapo malori 600 ya Tanzania yamekamatwa na kuzuiliwa kwa kipindi cha miezi miwili.

Zambia iliyakamata malori hayo yalipokuwa yakirudi kutoka DR Congo ambapo yalikuwa yameenda kubeba mbao.

Rais wa Zambia Edgar Lungu siku ya Jumatatu alisema kuwa hatokubali taifa lake kutumika kama kituo cha miti ya mbao akidai kuwa madereva wa malori kutoka Tanzania wanakiuka sheria kuhusu usafirishaji mbao.

Maafisa wa Tanzania wametoa wito kwa maafisa wao katika ubalozi wao nchini Zambia kuwasilisha swala hilo na maafisa husika ili kupata suluhu ya haraka.

Muungano wa madereva wa malori wa Tanzania Tatao umesema kuwa wanachama wake walifuata maelezo yote kuhusu ununuzi na mauzo ya nje ili kuweza kuingia nchini DR Congo.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu