Mamia ya wafanyakazi kutoka katika kikosi cha kupambana na majanga ya moto wanapambana ili kuudhibiti moto mkubwa uliozuka katika msitu mkubwa katikati mwa Ureno, ambao umeua watu sitini mpaka sasa.

In Kimataifa
Mamia ya wafanyakazi kutoka katika kikosi cha kupambana na majanga ya moto wanapambana ili kuudhibiti moto mkubwa uliozuka katika msitu mkubwa katikati mwa Ureno, ambao umeua watu sitini mpaka sasa.
Inaarifiwa kuwa watu wengi walifia katika gari zao wakati walipokuwa katika harakati za kuondoka katika eneo la tukio wilayani Pedrógão Grande.
Akizungumza baada ya kutembelea eneo la tukio, waziri mkuu nchini humo , Antonio Costa, amesema kwamba wazima moto wamekwisha dhibiti mioto zaidi ya miamoja na hamsini nchini mwake.
Waziri Antonio ametangaza siku tatu za maombolezo na kueleza kuwa ni janga kubwa kwa nchi yake, kutoakana na kukabiliwa na majanga ya mioto mikubwa inayozuka katika misitu mikubwa miaka ya karibuni .
Vikosi viwili vya jeshi vimepelekwa katika eneo la tukio ili kuongeza nguvu na kutoa msaada wa dharula.
Umoja wa Ulaya,Ufaransa na Hispania kwa pamoja wamejitolea kutoa msaada wowote utakao hitajika, ikiwemo ndege za kupambana na mioto mikubwa kama hiyo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu