Mamlaka za maji na mabonde zaimizwa kubuni vyanzo vipya vya mapato.

In Kitaifa

Serikali imezihimiza Mamlaka za maji na mabonde ya maji kubuni vyanzo vipya vya mapato, vitakavyosaidia kujiendesha vyenyewe bila kutegemea serikali kuu.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Profesa Kitila Mkumbo alipokuwa akizungumza na watumishi wa mamlaka ya maji Singida (SUWASA), Bonde la maji kanda ya kati na Maabara .

Amesema kuwa Serikali haina fedha za kukidhi mahitaji yote ya mamlaka za maji na mabonde nchini, hivyo ni vyema vikaweka mikakati ya kujitengemea kimapato.

Aidha, Katibu Mkuu amewataka watumishi wa SUWASA, kutoa huduma bora itakayovutia wananchi wengi zaidi kupata huduma ya maji katika mamlaka hiyo.

Hata hivyo, Katika hatua nyingine, Prof. Mkumbo ametumia nafasi hiyo kusisitiza utaratibu wa kulipia kwanza maji (pree paid), kabla ya kupata  huduma ya maji.

Kwa upande wake Afisa Maji bonde la kati, Benard Chikarabhani amesema kuwa wameanza utekelezaji wa ujenzi wa bwawa la Farkwa, kwa lengo la kuongeza usambazaji wa maji katika mji wa Dodoma, Bahi, Chamwino na halmashauri ya wilaya Chemba.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu