Mamlaka za maji na mabonde zaimizwa kubuni vyanzo vipya vya mapato.

In Kitaifa

Serikali imezihimiza Mamlaka za maji na mabonde ya maji kubuni vyanzo vipya vya mapato, vitakavyosaidia kujiendesha vyenyewe bila kutegemea serikali kuu.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Profesa Kitila Mkumbo alipokuwa akizungumza na watumishi wa mamlaka ya maji Singida (SUWASA), Bonde la maji kanda ya kati na Maabara .

Amesema kuwa Serikali haina fedha za kukidhi mahitaji yote ya mamlaka za maji na mabonde nchini, hivyo ni vyema vikaweka mikakati ya kujitengemea kimapato.

Aidha, Katibu Mkuu amewataka watumishi wa SUWASA, kutoa huduma bora itakayovutia wananchi wengi zaidi kupata huduma ya maji katika mamlaka hiyo.

Hata hivyo, Katika hatua nyingine, Prof. Mkumbo ametumia nafasi hiyo kusisitiza utaratibu wa kulipia kwanza maji (pree paid), kabla ya kupata  huduma ya maji.

Kwa upande wake Afisa Maji bonde la kati, Benard Chikarabhani amesema kuwa wameanza utekelezaji wa ujenzi wa bwawa la Farkwa, kwa lengo la kuongeza usambazaji wa maji katika mji wa Dodoma, Bahi, Chamwino na halmashauri ya wilaya Chemba.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu