Manji adai kuwa bado yeye ni Diwani halali.

In Kitaifa, Siasa

 

Mfanyabiashara Yusuf Manji ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo kuwa, yeye bado ni Diwani wa Kata ya Mbagala Kuu.

Manji amedai kuwa hatambui kuvuliwa udiwani kama ilivyotangazwa na Mstahiki Meya wa Temeke Abdallah Chaulembo September 6 mwaka huu.

Manji ametoa malalamiko hayo kwenye kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili na wenzake mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shaidi.

Katika kesi hiyo ambayo Wakili wa Serikali Mwandamizi Mutalemwa Kishenyi, amedai upelelezi haujakamilika na Manji kudai ameona habari kupitia gazetini kuwa amevuliwa udiwani.

Amedai kama ni kweli amevuliwa Udiwani hatambui, kwani ana miezi 2 yupo gerezani na serikali inatambua kwamba yeye ni Diwani.

Pia Manji amedai kama hilo haliwezekani, basi wamuandikie barua itakayoonyesha agenda ya vikao vyote na yeye atazijibu kwa njia ya barua pia.

Aidha amedai hiyo kesi ni nzito na DPP hapaswi kuangalia upande wake wa kesi tu, kwani yeye amechaguliwa na wananchi na anawasaidia.

Awali kabla ya kuelezwa hayo Wakili wa utetezi Seni Malimi, alidai wanatarajia kuwasilisha maombi ambayo ni ya siri katika tarehe ijayo.

Baada ya kuelezwa hayo Hakimu Huruma Shaidi akautaka upande wa mashtaka kuhakikisha wanalifanyia kazi suala hilo, ambapo kesi imeahirishwa hadi September 18 mwaka huu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu